Saturday, March 21, 2020

Je, Mauricio Pochettino ndiye mwokozi?


Kocha wa klabu Manchester United, Ole Gunnar anafahamu kuwa kitoweo chake kinaweza kupigwa teke wakati wowote. Aliyekuwa kocha wa Totenham Hotspurs, Mauricio Pochettino anatarajiwa kumridhi Ole atakapo pigwa kalamu mwishoni mwa msimu huu. Baada ya Manchester United kumsajili kiungo wa kireno, Bruno Fernades mwezi Januari huenda klabu hii ikkajirejeshea heshima yake  hivi karibuni. Hatahivyo, kuna jina moja linalokosekana ugani Old Trafford ili maazimio hayo yatimie; Mauricio Pochettino

Mauricio Pochettino
Poch alikuwa kwenye mchuano baina ya klabu ya Leeds na Brendford hivi maajuzi jambo lilozua mtafaruku pale nchini Uingereza hasa kwenye kambi ya Klabu ya Manchester United. Pochettino alisaidia klabu ya Tottenham Hotspurs kufika kwenye fainali ya Michuano ya klabu bingwa barani ulaya msimu uliopita kabla ya kupigwa kalamu msimu huu.
Katika Michuano yake, Pochettino alipendea sana mfumo wa 4-3-1-2. Alimpa nahodha wa timu ya taifa ya Uingereza, Harry Kane  majukumu ya kucheka na wavu kwa usaidizi wake Dele Alli. Je, Klabu ya Manchester  united ina wachezaji wa hadhi yake Harry Kane pamoja na Dele Alli?  Kwenye mfumo wake Pochettino alipendelea sana kumtumia Mkenya Victor Wanyama kama kiungo wa kati kwa usadizi wake Harry
Wings na Mousa Sissoko. Paul Pogba pamoja na Bruno Fernades wanauwezo huo?
Kwenye safu ya Ulinzi  Pochettino aliwapendelea walinzi wakibelgiji, Tobby Alderwield pamoja na Jan Vertogen  huku wakisaidiwa naye Danny Rose pamoja na Serge Aurier. Kwa kuangazia kikosi cha Manchester United ambacho kinaogozwa na beki ghali Zaidi ulimweguni, Harry Maguire kina uwezo wa hali ya juu kuliko kikosi alichotumia Pochettino pale Totenham Hotspurs. Jambo hili linawapa mashabiki wengi wa Manchester United Imani kuwa Pochetinho anauwezo wa kuirejeshea Manchester United hadhi yake iwapo atapewa nafasi hio.
Tukilinganisha Vikosi hivi viwili ni kweli kwamba Manchester United ya sasa ni moto wa kuotea mbali ila imekosa kocha wa kuielekeza vilivyo. Je, Mauricio Pochettino ataibadilisha Manchester United?
@Albanus_10

No comments:

Post a Comment